• LOGIN
  • No products in the cart.

LSC: MADA KUU 1.4 WANYAMA NA NDEGE

LSC: MADA KUU 1.4 WANYAMA NA NDEGE

Goats | Farm Animals - Farm Sanctuary          Long Island Cow Who Escaped From Manorville Farm Captured              How To Integrate Ducks and Chickens

African lion, facts and photos    Amur tiger - Saint Louis Zoo  949,580 Birds Stock Photos - Free & Royalty-Free Stock Photos from  Dreamstime

Utangulizi

Nchi ya Uganda ina utajiri mwingi kutokana na wanyama na ndege wa aina mbalimbali. Baadhi ya Wanyama hawa ni wa nyumbani na wengine ni wa porini. Vilevile, baadhi ya ndege hawa ni wa nyumbani na wengine ni wa porini. Je, kuna wanyama wowote unaojua? Ni wanyama gani wa nyumbani unaojua? Je, kuna wanyama wa porini unaojua? Je, Wanyama hao wana umuhimu gani kwa jamii? Unajua umuhimu wa ndege kwa jamii?

Funzo a: Kutambua majina ya wanyama na ndege wa nyumbani

Shughuli 1.4: Kusikiliza na kuzungumza

1. Katika vikundi;

(a) Jadiliana kuhusu wanyama wa nyumbani na kisha kila kikundi kitaje majina ya wanyama waliojadiliana.
(b) Jadiliana kuhusu ndege wa nyumbani na kisha kila kikundi kitaje ndege waliojadiliana.
(c) Tazameni michoro ya wanyama iliyopo hapa chini na kila mmoja ataje majina ya wanyama hao. Chagua jina sahihi kutoka yale uliyopewa katika boksi hapo chini.

WANYAMA WA NYUMBANI

Ng’ombe                                         Mbuzi                                     Punda

How to determine when a cow is in heat - Farm and Dairy    Boy Bands are Back! Banding Goats 101 - Backyard Goats    Donkey - Wikipedia

Farasi                                                  Kondoo                                      Sungura

How Far Can a Horse Travel? Horse Running Endurance Explained    Facts About Sheep | Live Science  Rabbit - Facts, Description, Food Habits, Pet Care and Pictures

2. Katika jozi,

(a) Kubalianeni kati yenu juu ya milio ya wanyama au ndege na kila mmoja wenu atoe milio ya wanyama wawili.

WANYAMA/NDEGE NA MILIO YAO

A                                                                      B

Mbuzi                                             Klaak-klaak

Kondoo                                           Kwaak-kwaak

Kuku                                              Mee-mee

Paka                                              Moo-moo

Mbwa                                            Bwoo-bwow

Bata                                               Baa-baa

Ng’ombe                                          miaw-miaw

b) Shirikiana kueleza umuhimu ndege wafuatayo.

FAIDA ZA WANYAMA WA NYUMBANI.

MNYAMA                                              FAIDA

a)  Mbuzi                                                    Nyama, maziwa ,ngozi, mbolea.

b)  Ng’ombe                                               Maziwa, nyama, mbolea,ngozi.

c)   Punda                                                   Kubeba mizigo,usafiri ,mbolea.

d)   Farasi                                                   Kubeba mizigo,usafiri,mbolea,michezo mbalimbali.

d)   Kondoo                                                Nyama,maziwa,sufu,ngozi,mbolea.

e)   Paka                                                     Kushika panya.

f)    Mbwa                                                  Ulinzi na usalama.

g)    Sungura                                              Nyama,mbolea.

h)    Nguruwe                                             Nyama ,mbolea

i)Ngamia                                                    Kubeba mizigo,usafiri,nyama,mbolea,ngozi.

Funzo b: WANYAMA NA NDEGE WA PORINI.

Simba                                              ndovu                                               Pundamilia

           

Fisi                                                      Sokwe                                                      Tumbili

Hyena | mammal | Britannica      What do chimpanzees eat? : Jane Goodall      Monkey - Wikipedia

wanyama na ndege wengine ni ;

ngiri ,chuimilia ,chui, twiga ,nyati,korongo ,bundi, tai ,mwewe ,kuku ,jogoo kifaranga ,batamzinga nk.

Funzo d: Kutambua vikembe mbalimbali.

VIKEMBE;

Hawa ni watoto wa wanyama. Vikembe ni pamoja na:

  Mnyama kikembe
1 Ngombe Ndama
2 mbuzi kibui
3 ndege Kinda
4 kipepeo Kiwavu
5 nzi Buu
6 Farasi Kitekli
7 Mamba Kigwena
8 paka Kinyaunyau/kipusi
9 Fisi Bakaya/kikuto
10 Ndovu kidanga
11 Mbweha nyamawa
12 Nyani kigunge
13 kondoo kibebe
14 Farasi /punda Nyumbu
15 Mbu kiluwiluwi
16 Kuku Kifaranga
17 Simba Shibili
18 Nyoka kinyemere
19 Mbwa Kilebu
20 Nyuki Jana
21 Njiwa Kipura
22 Sungura kitungule
23 Papa Kinengwe

Shughuli 4.4: Kusikiliza, kuzungumza, kusoma na kuandika

(a) Katika jozi, tumieni kamusi, maktaba au mtandao kutafiti kuhusu vikembe mbalimbali. Baada ya utafiti, kila jozi liwasilishe majina ya vikembe darasani mbele ya wanafunzi wengine darasani.
(b) Katika vikundi, jadiliana na kuandika majina yaa vikembe na kila kikembe andikeni jina la mzazi wake.

Funzo e: Kusoma Makala kuhusu sifa za wanyama na ndege.

wanyama wengi wanatembea katika vikundi.

wanyama wanakula.

wanyama wanafa.

wanyama wanazaa.

wanyama wanapenda.

Ndege wanaweka mayayi.

Faida za wanyama wa nyumbani

Wanyama wa nyumbani ni wale ambao wanakubali kufugika na kuridhiana na mwanadamu katika mazingira ya kinyumbani, bila ya madhara mabaya.
Wanyama hawa wafugwao wana faida chungu nzima kwa mwanadamu; kuna ngamia, ng’ombe, mbuzi, mbwa paka, sungura na wengineo. Miongoni mwao wamo waliwao na wale wasioliwa, ingawaje wasioliwa pia wana umuhimu wao mwingi kwa mwanadamu; kama vile mbwa ni mlinzi madhubuti, farasi naye ni hodari kwa ubebaji wa mizigo na
usafiri. Paka ni msasi wa panya pamoja na faida nyingine nyingi.

Ama wale waliwao tukianza na ng’ombe ana manufaa makubwa katika harakati za ulimaji. Pakosekanapo trakta basi yeye huingia kazi, huchangia sehemu kubwa ya uchumi na maendeleo katika kilimo na ufugaji. Na kama ilivyo kawaida kuwa nyama zao ni kitowe, huliwa na kuuzwa pamoja na kutupa maziwa. Ngozi kama za ngamia, ng’ombe na mbuzi huleta pesa nyingi, kwani ni mali ghafi ya vifaa vingi kama vile viatu, mabegi, mikanda, majaketi, kofia, foronya za viti na kadhalika.

Ufugaji wa wanyama wote wa nyumbani waliwao na wasioliwa ni kitega uchumi kikubwa ambacho huleta maendeleo ya kiuchumi kwa mfugaji binafsi na taifa kwa ujumla.

Shirikiana na wenzako kujibu maswali

(a) Unaelewa nini kuhusu wanyama wa nyumbani kulingana na taarifa hii?
(b) Taja wanyama watano wa nyumbani waliwao.
(c) Taja wanyama watatu wa nyumbani wasioliwa.
(d) Eleza faida tatu za ng’ombe.
(e) Ni vitu gani ambavyo hutengenezwa kwa ngozi za wanyama?

Sarufi:

Funzo f: Kutumia vivumishi vimilikishi katika sentensi

Shughuli 6.4: Kusoma na kuandika

Katika makundi;

i. Jadiliana na kutambua maana ya vivumishi vimilikishi huku mkitoa mifano.
ii. Tumieni vivumishi vimilikishi mlivyotambua katika i. hapo juu kutunga sentensi mkitumia nomino za a-wa zinazotaja wanyama na ndege.

Funzo g: Kutumia vipatanishi vya nomino za ngeli ya a-wa katika sentensi

Nomino (umoja) vimilikishi Nomino(wingi) vimilikishi
MbwaBataNg’ombe

Mbuzi

Simba

WanguWakoWenu

Wetu

Wao

wake

MbwaBataNg’ombe

Mbuzi

Simba

WanguWakoWenu

Wetu

Wao

wake

Shughuli 7.4: Kusoma na Kuandika

Mkiwa katika vikundi,
i. Jadiliana kuhusu nomino za ngeli ya a-wa zinazotaja majina ya wanyama na ndege na kisha mziandike nomino hizo katika madaftari yenu.
ii. Tungeni sentensi sahihi kwa kutumia vipatanishi vya kisarufi vya ngeli ya a-wa. Sentensi hizi ziandikwe kwa chati kwa umoja na wingi na kutundikwa ukutani ili vikundi vingine vilinganishe na zao.

Funzo h: Kuandika insha kutokana na ufasiri wa michoro.

Shughuli 8.4: Kuandika.
a.Mada ikibadilika na kuwa “ndege wa porini wana umuhimu mkubwa kwa jamii” Eleza hoja ambazo utatoa kuunga mkono mada hiyo.
b Tunga sentensi tano katika wakati uliopo kwa kutumia majina ya wanyama na kisha uzigeuze sentensi hizo kwa wingi.

Muhtasari wa mada
Katika mada hii, umejifunza kuhusu,

a. majina ya wanyama na ndege wa nyumbani na porini.
b. faida za wanyama na ndege.
c. vikembe mbalimbali.
d. kusoma na kujadili makala yanayohusu sifa za wanyama na ndege.
e. matumizi ya vivumishi vimilikishi katika sentensi.
f. upatanishi wa kisarufi wa ngeli ya A–WA katika sentensi.
g. kuandika insha ya mwongozo kwa kufasiri michoro kuhusu wanyama na faida zao.

 

Courses

Featured Downloads